Jumatatu, 9 Septemba 2013

HOJA CHANYA KINANA SONGA MBELE

 




NA BASHIR NKOROMO
WALIOBOBEA katika medani ya falsafa husema, adui yako siyo lazima awe yule anayekunyooshea silaha ili kudhuru mwili au maisha yako, bali hata asiyekutakia mafanikio mema na kupuuza harakati zako za kimaendeleo ni adui tena namba moja.
Kwa mujibu wa wanafalsafa hao, tofauti na adui wa kukudhuru mwili au maisha yako ambaye akikushikia silaha unamtambua mara moja, asiyekutakia mema na kupuuza harakati zako za kimaendeleo, inakubidi uwe mweledi sana kumtambua haraka.
Wanasema, moja ya dalili za adui wa aina hiyo, ni yule ambaye ukifanya jambo linalokupeleka kwenye mafanikio makubwa analiponda kuwa halifai, na ukifanya baya linalokudidimiza anakusifia kwamba hilo ndilo zuri na la maana kuendelea nalo.
Ushauri unaotolewa na wanafalsafa hao, ni kwamba, ukishamtambua mtu kuwa ni adui yako, ukimsikia anakusifu kuwa jambo fulani unalofanya ni nzuri achana nalo mara moja, lakini akiliponda kwa nguvu zake zote kuwa unalofanya halina manufaa na kwamba ni la hovyo sana, basi jambo hilo ni jema, endelea kulifanya, yaani songa nalo mbele.
Katika gazeti moja la Raia Mwema, ambalo nimetokea kuliamini sana kuwa ni moja ya magazeti mahiri nchini na bila shaka nitaendelea kuamini hivyo, katika toleo lake la Novemba  28, mwaka huu, Mwandishi mmoja Evarist Chahali ambaye ameandika uchambuzi wake akiwa Uskochi, amejaribu kuandika uchambuzi alioupa kichwa cha  'Kosa la Kwanza kwa Kinana'.
Katika mtiririko wa uchambuzi huo ameeleza mengi akimsadifu Kinana hadi na wanasiasa za Marekani. Lakini  kwa kuwa sina muda na nafasi ya kutosha ya kukuchosha msomaji kwa kuyarejea aliyoandika, afadhali nijadili naye kuhusu jambo moja tu alilojaribu kulifanya jamii ilione kuwa ni kosa la kwanza alilofanya Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, wakati wa mkutano wa CCM, uliofanyika mjini Geita wiki iliyopita.
Chahali anajaribu kushawishi wasomaji wakubaliane nake kwamba hatua ya Kinana kukabidhi leseni kwa wachimbaji madini wadogo 21, kwenye machimbo ya Mugusu, wakati wa mkutano huo eti ilikuwa ni aina ya kuhodhi mamlaka ya Wizara ya Nishati na Madini inayoratibu na kusimamia shughuli za madini nchini ikiwemo uchimbaji.
Tena anaenda mbali zaidi kwamba, kwa Kinana kufanya hivyo, inaweza kutafsirika kuwa ni mwendelezo wa vitendo vya kifisadi kwenye sekta ya madini hapa nchini, akisema kwamba huenda waliokabidhiwa leseni zile siyo wamiliki halisi wa leseni hizo, kwamba ni mamluki waliozipokea leseni hizo wakiwa ni vivuli vya watu wengine.
Pangine, hili la uwezekano wa kwamba waliopewa leseni walikuwa vivuli vya wengine, nisilisemee sana, kwa kuwa inawezekana. Lakini ili kulithibitisha hilo ni lazima anayetuhumu hivyo ajiridhishe kwa kujiuliza kwamba inawezekanaje hao wachimbaji wadogo 21, wawe mazuzu kiasi cha kushangilia kuzipokea leseni hizo wakati wanajua siyo zao, hasa ikizingatiwa kwamba hao ni miongoni mwa wakazi wa Geita ambao kilio chao cha kila siku ni kupata leseni za uchimbaji mdogo kwenye eneo hilo la Mgusu?
Na kama pengine walilipwa ili kuzipokea, mamia ya watu waliokuwa kwenye mkutano ule nao walishawishika vipi hadi nao wakashangilia hatua hiyo badala ya kuzomea? Maana waliokuwa kwenye mkutano huo wanawajua wote waliopakabidhiwa leseni hizo kwa sababu wote ni wakazi wa Geita.
Mimi ni miongoni mwa mamia ya watu waliokuwa kwenye mkutano huo  wa hadhara wa CCM ambao Kinana akikabidhi leseni hizo.
Ni kwamba, Wizara ya Nishati na Madini ilikuwa imeshapitia taratibu zote za kutoa leseni hizo, na kilichofanyika pale ni tukio la kukabidhi leseni tu, kama vile Mkuu shule ya  Sekondari, Chuo cha Ufundi au Chuo Kikuu, ambavyo huandaa vyeti kwa ajili ya wahitimu kisha kazi ya kuwakabidhi wanaostahili ikafanywa na mgeni rasmi aliyealikwa kwenye mahafali.
Hivi Chahali na wengine wenye mtazamo kama yeye (kama wapo), kama mgeni rasmi akikabidhi hivyo vyeti kwa wahitimu waliostahili kwa kufuzu kwa vigezo, ndiyo inamaanisha kwamba amepora mamlaka ya shule au chuo husika?
Maana katika mkutano ule, ambao bila shaka asiye itakia mema CCM ulimkera, Watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini, kama Taasisi ya serikali inayotekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi kilichopewa na wanachi ridhaa ya kuunda serikali, walikuwepo kutokana na kuitwa na mwajiri wao CCM ili kueleza wanavyosimamia kwa manufaa ya umma sekta ya madini.
Ili waweze kueleza vizuri mbele ya wananchi, ilikuwa ni lazima waje na ushahidi wa kutosha kuwaridhisha wananchi hao na mwajiri mwenyewe (CCM) juu ya usimamizi huo katika rasilimali hiyo adhimu Tanzania.
Chama Cha Mapinduzi ambacho ndicho chenye mkataba na wananchi tangu uchaguzi mkuu uliopita, kilikuwa tayari kina malalamiko kwamba wakazi wa Geita wanapata dhiki kutokana na kutopewa fursa ya kuruhusiwa kufanya uchimbaji mdogo katika mgodi wa Mugusu.
Sasa kwenye mkutano akaja Naibu Waziri wa Nishati na madini anayeshughulikia madini, Steven Masele. Alifika kuitika wito wa CCM yaani mwajiri wa serikali iliyopo madarakani, Kinana, kisha akapandishwa jukwaani  akahojiwa mbele ya wananchi, Je bwana mmefikia wapi katika kutatua kero hii ya wachimbaji wadogo? Masele akajibu " Tunazo leseni 21 kwa ajili ya wachimbaji wadogo waliofaulu vigezo ambazo tunaweza kuwakabidhi wakati wowote.
Kinana akamuuliza Masele " Je, leseni hizo zimepitia utaratibu wote vizuri na zipo tayari kuweza kukabidhiwa kwa hao wachimbaji? Masele akajibu, "ndiyo".
Baada ya hapo Naibu Waziri akamuomba Kinana kuwakabidhi leseni zao wahusika. Kinana akafanya kazi hiyo ikakamilika bila malalamiko, maana ilifuatiwa na nderemo na vifijo kwa waliopewa leseni hizo na pia kwa wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Kimsingi mtiririko mzima wa kukabidhi hati hizo ulikuwa hivyo, lakini cha kushangaza ni kwamba mchambuzi wa makala hiyo, Chahali amejaribu, kutengeneza mawazo yananyowafanya baadhi ya wasomaji wake wadhanie leseni zile zilitolewa ghafla, papo hapo na CCM!
Bila shaka Chahali amebahatika kusoma na kuhitimu masomo yake, na bila shaka wakati wa mahafali alikabidhiwa cheti na mgeni rasmi, siyo Mkuu wa Chuo. Je, wakati anapokea cheti hicho alisita kwa kuhofia kwamba kwa mgeni rasmi kumkabidhi cheti hicho alikuwa anapora mamlaka ya mkuu wa chuo?
La msingi hapa ni kwamba,  hatua ya Katibu Mkuu wa CCM, Kinana kuwakabidhi leseni wachimbaji hao wadogo halikuwa na ukiukwaji wowote na lilikuwa jema kwa CCM, ndiyo sababu kalamu za wasioitakia mema CCM wanaotamani wakiamka wakute imeondoka madarakani zimekemea tena kwa ukurasa mzima kwamba lilikuwa tukio baya na kosa la kwanza kwa katibu Mkuu huyo.
Kwa mtazamo wangu na kwa kuzingatia ushauri wa wanafalsafa, Kinana usiungame kwamba ulilofanya ni kosa la kwanza, isipokuwa ni moja ya matukio bora ya kwanza uliyofanya katika ziara yako ya kwanza tangu uteuliwe kuwa Katibu Mkuu wa CCM mapema mwezi huu kule mjini Dodoma.
Songa mbele, huku ukijitahidi kutojaribu kufanya hata moja ambalo hao wasioitakia mema CCM (ambao kwa dalili zao unawajua) watakusifu. Na siku ukiteleza ukalifanya jambo ukasikia wamekusifu hadharani, lichunguze kwa makini na uliache mara moja, usiendelee nalo.
Posted by CCM Blog
 

KINANA, NAPE KUWASILI SHINYANGA KESHO SAA TATU ASUBUHI






KINANA, NAPE KUWASILI SHINYANGA KESHO SAA TATU ASUBUHI
Sep 9, 2013
Ndugu Kinana
SHINYANGA, Tanzania
KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana kesho Jumanne, ataanza ziara ya siku nne mkoani Shinyanga kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM na uhai wa Chama.

Taarifa ilizopata theNkoromo Blog zimesema akiwa mkoani Shinyanga Kinana atakagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika wilaya zote za mkoa huo sambamba na kutoa kadi kwa wanachama wapya wa CCM ambapo pia atafanya vikao vya ndani ikiwa ni moja ya mikakati ya uimarishaji wa chama mkoani humo.

Katibu wa CCM mkoani Shinyanga, Adam Ngalawa amesema leo kwamba Kinana na msafara wake akiwemo Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, CCM, Nape Nnauye, wanatarajiwa kupokelewa kesho saa 3 asubuhi katika kata ya Isaka wilayani Kahama wakitokea Nzega mkoani Tabora.

Ngalawa alisema baada ya kupokelewa kwa Katibu Mkuu akiwa katika kata ya Isaka atasaini kitabu cha wageni na kisha atapokea taarifa ya utekelezaji wa kazi za CCM za wilaya ya Kahama na mkoa kwa ujumla pamoja na taarifa ya serikali ya mkoa.

Akiwa katika kata hiyo Kinana atagawa kadi za CCM kwa wanachama wapya na kisha atawasalimia wananchi kabla ya kuelekea katika kata ya Mwendakulima ambako atakagua miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya cha Mwendakulima.

Katibu mkuu huyo akiwa mjini Kahama atafanya shughuli mbalimbali ikiwemo kuweka jiwe la msingi katika ofisi ya CCM kata ya Majengo, kufungua shina la wakereketwa la Mkombozi SACCOS Majengo pia atakuwa na kikao cha ndani na viongozi wa kata, matawi, mabalozi, wazee na madiwani wa CCM wilayani Kahama.

Kesho mchana Kinana atakuwa na mkutano wa hadhara katika eneo la uwanja wa CDT ambapo keshokutwa jumatano ataelekea wilaya ya Shinyanga ambako atakagua shughuli mbalimbali za maendeleo katika wilaya hiyo na kushiriki katika ujenzi wa hospitali ya wilaya hiyo pia atakuwa na mkutano wa hadhara katika kijiji cha Salawe.

Pia katibu huyo ataendelea na ziara yake katika wilaya za Kishapu na Shinyanga manispaa ambako pia atakuwa na shughuli za kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo kama ilivyoainishwa ndani ya ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010.

Kinana ataondoka mkoani Shinyanga Septemba 14, mwaka huu kwenda katika mkoa mpya wa Simiyu ambako pia atafanya shughuli za kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM na uimarishaji wa chama katika wilaya zote za mkoa huo.
Imetayarishwa na theNkoromo Blog




KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AWASILI NZEGA


 


KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AWASILI NZEGA, APOKEA PIKIPIKI 9 KUTOKA KWA DK. KHAMIS KIGWANGALA NA KUKABIDHI KWA KATA 9 ZA CCM
Monday, September 9, 2013
1Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Siasa Ndugu Nape Mosses Nnauye ukiwasili katika mji wa Nzega Katika wilaya hiyo Tayari kwa kuanza Ziara ya Siku 18 katikia mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara kesho ambapo ziara hiyo itaanza katika mkoa wa Shinyanga, Katibu Mkuu huyo amepokelewa na viongozi mbalimbali wa chama na wananchi waliojitokeza katika mapokezi hayo, Kinana leo amezungumza na wananchi wa Nzega na kukutana na vikundi mbalimbali vya ujasiriamali ambapo pia amepokea Pikipiki tisa kutoka kwa mbunge wa jimbo hilo Dk. Khamis Kigwangala ambazo ambazo amezikabidhi kwa viongozi wa kata 9 kati ya 21 zilizopo katika Wilaya hiyo, ambapo pia amekabidhi mashine ya kutotolea vifaranga vya kuku kwa kikundi cha wazee wa Nzega , Pikipiki hizo zimekabidhiwa katika kata za Budushi, Ndala, Puge, Nkininziwa,Mbogwe, Lusu, ,Ijaniga, Utwigu na Isanzu baadae pikipiki 7 zitafutaiwa na kisha kata tano za mwisho. PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-NZEGA 2Vijana waendesha pikipiki na baiskeli wakiongoza msafara wa Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. 3 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa skafu mara baada ya kuwasili wilayani Nzega leo 4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipita katikati ya vijana wa Greenguard wa CCM huku wakitoa heshima zao mble ya mgeni huyo mara baada ya kuwasili wilayani Nzega leo. 5Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na viongozi mbalimbali. 6 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wanachama mbalimbali na wananchi mara baada ya kuwasili wilayani Nzega. 7Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi 8 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisamewa risala wakati alipozindua mradi wa ujenzi wa vibanda vya biashara vya mradi wa Chama cha Mapinduzi Wilayani Nzega. 9Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua mradi wa ujenzi wa vibanda vya biashara katika uwanja wa Samora, vibanda hivyo ni mradi wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilayani Nzega. 10Mbunge wa Jimbo la Nzega Khamis Kigwangala akizungumza na wananchi huku Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza. 11Katibu wa Itikadi, Uenezi na Siasa Ndugu Nape Mosses Nnauye huku katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akipiga makofi 12 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi huku Mbunge wa Jimbo la Nzega Khamis Kigwangala akimsikiliza. 13Wananchi wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika mapokezi hayo 14Wananchi wa Nzega wakiimba kwa furaha mara baada ya kumpokea katika mkuu wa CCM Ndugu Abdurahman Kinana. 15Umati wa wanavikundi wakiwa katika mkutano huo 17Mbunge wa Jimbo la Nzega Khamis Kigwangala akimsikiliza akiongea na wananchi 18Pikipiki zilizotolewa na Mbunge wa Jimbo la Nzega Khamis Kigwangala akimsikiliza zikiwa tayari kwa ajili ya kukabidhiwa. 19 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijaribu kuendesha moja ya pikipiki kbaada ya kuzikabidhi kwa viongozi wa Kata 9 za Wilaya ya Nzega, 20Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi pikipiki kwa Hanifa Musa Kutoka kata ya Isanzu huku Mbunge wa Jimbo la Nzega Khamis Kigwangala katikati akishuhudia tukio hilo. 21 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpongeza Mbunge wa Jimbo la Nzega Dk. Khamis Kigwangala mara baada ya kukabidhi mashine ya kutotolea vifaranga kwa kikundi cha wazee wa Nzega mjini humo.22Katibu wa Itikadi, Uenezi na Siasa Ndugu Nape Mosses Nnauye akizunumza na wana Nzega. 23Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizunumza na wananchi wakati alipowaambia hakuna haja ya kubadilisha mbunge mara kwa mara katika uchagzi kama mbuge aliyepo anafaa na anawatumikia wananchi vizuri kama vile Dk. Mbunge wa Jimbo la Nzega Khamis Kigwangala



NDG. KINANA NA NAPE ZARANI MIKOA YA SHINYANGA, SIMIYU NA MARA



Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahaman Kinana septemba 10 anatarajiwa kuanza ziara ya kawaida katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara.

Ziara hiyo itaanzia katika mkoa wa Shinyanga septemba 10 mpaka 13 mwaka huu, kwa kutembelea wilaya zote nne za mkoa huo na kufuatiwa na mkoa mpya wa Simiyu kuanzia Septemba 14 mpaka septemba 19 kwa kutembelea wilaya zote tano Kabla ya kuhitimisha ziara hiyo kwa kutembelea wilaya Sita za mkoa wa Mara kuanzia Septemba 20 Mpaka 25 mwaka huu.

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu wa CCM ataambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye.

Kwa mujibu wa Ratiba ya ziara hiyo, Wajumbe hao wa sekretarieti watakagua uhai wa Chama ikiwa ni pamoja na kupokea wanachama wapya sanjari na kuhamasisha wananchi kujituma katika shughuli za uzalishaji ili Kuleta tija katika maisha Yao na ya taifa kwa ujumla.

Aidha watakagua maendeleo ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010/2015 hasa katika miradi ya kimaendeleo Kama vile Ujenzi wa majosho kwa ajili ya wafugaji, maendeleo ya maboresho ya kilimo cha Pamba, uvuvi wenye tija pamoja na maboresho ya sekta za Afya, elimu na miundombinu zikiwemo Barabara.

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu  atapata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kwa kushauriana na serikali kutafuta namna ya kuzitafutia ufumbuzi.Katibu mkuu pia atafanya mikutano ya ndani, na ya hadhara katika kila wilaya za mikoa hiyo.

Imetolewa na;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi
05/09/2013
 
 



 
 
Hakuna maoni:

Jumapili, 8 Septemba 2013

MBIO ZA BENDERA


NAPE AZINDUA MBIO ZA BENDERA



 Wamama kutoka mkoa wa Iringa wakicheza ngoma ya kihehe wakati wa uzinduzi wa Mbio za Bendera.

 Wanachama na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi wakishangilia salaam walizokuwa wanapewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Ndugu Sixtus Mapunda.
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Sixtus Mapunda akisalimia wakazi wa Ruaha Buyuni wakati wa uzinduzi wa  wa Mbio za Bendera ya Chama mkoani Iringa
 Wananchi akifuatilia kwa makini hotuba za viongozi wa chama waliofika wakati wa uzinduzi wa Mbio za Bendera ya Chama mkoani Iringa.
 Viongozi wa Chama mkoani iringa wakifuatilia ratiba ya matukio mbali mbali yaliyopangwa wakati wa uzinduzi wa mbio za Bendera ya Chama Mkoani Iringa.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akifungua Bendera ya Chama tayari kwa kuanza kwa mbio za Bendera ya Chama .
 Vijana wakakamavu wa chama wakiwa wamebeba picha ya Mwenyekiti wa Chama ambayo itakimbizwa sanjali na Bendera ya Chama katika mkoa wa Iringa.

 Bendera na Picha ya Mwenyekiti ambazo lengo ni kuwakumbusha wana CCM kukilinda na kukitetea chama ikiwa pamoja na kuwaeleza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi.


Katibu wa CCM mkoa wa Iringa ndugu Emmanuel Mteming'ombe akitoa salaam za utangulizi wakati wa uzinduzi wa Mbio za Bendera.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu akihutubia wakazi wa Ruaha Mbuyuni wakati wa uzinduzi wa mbio za Bendera ya chama mkoani hapo

 Katibu wa NEC Itikad na Uenezi akihutubia wakati wa Iringa ambapo aliwaambia mbio hizo zitawasaidia wakazi wa mkoa huo kuelewa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi, kukilinda na kujenga chama.
 Katibu wa NEC akikabidhi mpira kwa moja ya timu zilizofanya vizuri.
 Katibu wa NEC akikabidhi vyeti vya kutambua mchango wa mabalozi wa nyumba kumi .

Bendera ya Chama ikiwa juu kama ishara ya kuwa mbio za Bendera zimeshaanza.
          

Hakuna maoni:

Alhamisi, 5 Septemba 2013

Kagame kiburi



                        Kagame kiburi
                                                                             September 1, 2013,


*Wanaompa jeuri sasa waanikwa, yamo mataifa makubwa
*Vyombo vya kimataifa vyatumika kumkingia kifua kila kona
*Uamuzi wa Kenya, Uganda, kujitoa bandari Dar wahusishwa

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Rwanda Paul Kagame bado anaonekana kuwa na kinyongo na Rais Jakaya Kikwete tangu alipopewa ushauri wa kukaa meza moja na waasi ili kumaliza migogoro iliyopo.

Hata hivyo imeelezwa kuwa Rais Kagame anaonekana kuwa na kundi nyuma yake ambalo linampa kiburi na kujiamini kwa kila anachokifanya na ndio maana hakuna mahali ambapo anaonesha kuwa tayari kutumia busara kumaliza tofauti iliyojitokeza.

Tayari Rais Kikwete ameweka wazi kuwa Serikali yake haipo tayari kuingia kwenye malumbano na Rwanda wala nchi nyingine yoyote na kwamba kuhusu Rwanda busara itatumika kutafuta ufumbuzi wake.

Kauli ya Rais Kikwete imekuja baada ya Rais Kagame kutoa kauli za kejeli baada ya kushauriwa na Rais Kikwete kuwa ni vema akakaa na vikundi vya waasi kutafuta ufumbuzi wa kumaliza migogoro nchini Rwanda, ushauri ambao unaonesha kutomfurahisha Kagame.

Wakizungumza wiki hii baadhi ya wachambuzi wa siasa za kimataifa, wameliambia Jambo Leo Jumapili kuwa Rais Kagame anaonekana kuwa na kiburi na hiyo inatokana na kutumia mataifa mengine kuonesha kukasirishwa kwake na ushauri wa Rais Kikwete.


Kwa mujibu wa wachambuzi hao, ni kwamba Rais Kagame anapata kiburi kwasababu pia kuna mataifa makubwa ambayo yanampa msukumo wa kutaka uhusiano wa nchi hizo mbili kuendelea kuwa kwenye kutetereka ingawa Serikali ya Tanzania imezidi kuweka wazi uhuasiano wa nchi hizo si mbaya kama ambavyo inaelezwa.

Kitendo cha Rais wa Rwanda Paul Kagame kutokuwa tayari kuumaliza mgogoro huo, mjadala mkubwa umezidi kuibuka kutokana na kutetereka kwa uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda huku Rais wa Paul Kagame akidaiwa kuwa ana kiburi ndio maana hadi sasa hajaonesha kutokuwa tayari kukaa kwenye mazungumo kutafuta muafaka

Wakizungumzia zaidi nguvu ya Rais Kagame, ni kwamba inawezekana pia inatokana  na namna ambavyo anatumia vyombo vya habari vya kimataifa kuelezea uhusiano wake na Tanzania.

Pia nguvu ya wanaomuunga mkono Rais Kagame imedaiwa kuwa ndio inayoendelea kumpa kiburi cha kutokuwa tayari kukaa na vikundi vya waasi kutafuta suluhu.

Wakati hayo yakiendelea duru za kimataifa zinafafanua kuwa Rais Kagame huenda anapata kiburi kutokana na kupewa nguvu na aliyewahi kuwa Rais wa Marekani Bill Clinton.

Siku za hivi karibuni baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa na mitandao ya kijamii vimemnukuu Clinton akitoa kauli za kumkingia kifua Rais Kagame.

Rais Kagame amekuwa akituhumiwa kufadhili kundi la waasi la M23 ambalo lipo kwenye mapigano ya muda mrefu nchini Congo lakini pia Clinton alinukuliwa akimtetea Rais Kagame na kumsafisha dhidi ya tuhuma hizo.

Hata hivyo Rais Kagame mwenyewe amekuwa akikanusha kuhusika kulifadhili kundi hilo kwa namna yoyote ile, na hilo amekuwa alisisitiza mara kwa mara inapotokea mataifa mengi kumtuhumu.

Taarifa zaidi kuhusu Rais Kagame, kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari vya kimataifa, vinadai kuwa mbali ya Clinton kumtetea  pia baadhi ya nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki nazo zinaonekana kumuunga mkono harakati zake za kuiendelea kutokuwa na uhusiano mzuri na Tanzania.

Miongoni mwa wanaotajwa kuwa nyuma ya Rais Kagame ni baadhi ya viongozi wa Serikali ya Uganda na hiyo inatokana na kile kinachoelezwa kuwa aliwahi kuwa  Mkuu wa Idara ya Usalama wa Rais Yoweri Museveni wa Uganda kabla ya kujiunga na chama cha RPF.

Ushirika huo wa Kagame kwa Rais Museveni, unatajwa kuwa ndicho kinachotafsiriwa sasa kwamba kinawafanya waendelee kushirikiana.

Pia ilibainishwa kwamba ushirika wa Marekani chini Clinton kwa Kagame, ulikuwa umeshika kasi na hivyo kufanya Taifa hilo kubwa Duniani kukiunga mkono chama cha RPF alimokuwa Kagame.

Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa katika baadhi ya mitandao ya kijamii, jeuri hiyo ya kuwa na vigogo wanaomkingia kifua, ndio inayompa uwezo Kagame kuendelea kuvuruga uhusiano baina ya nchi yake na baadhi ya nchi nyingine ikiwemo Tanzania.

Taarifa zaidi zilidai kuwa hata kitendo cha Rwanda kuamua kujitoa kutumia Bandari ya Dar es Salaan kupitisha mizigo yao ikiwa ni sehemu ya kuonesha hasira zake dhidi ya Tanzania.
Mbali ya Rwanda pia Uganda na Kenya nazo zimejiondoa kutumia bandari hiyo na sasa wamepanga kutumia bandari ya Mombasa.

Kabla ya uamuzi huo wa kujiondoa nchi za Uganda na Rwanda zilikuwa zikitumia bandari ya Dar es Salaam kama kituo cha kupitishia mizigo yao.

Uamuzi wa kutotumia bandari ya Dar es Salaam kwa nchi hizo unaanza leo (Septemba Mosi), unafanyika baada ya mazungumzo ya faragha yaliyomshirikisha Rais Kagame na Rais Museveni na Serikali ya Kenya.

Wakati hayo yakiendelea, Watanzania na Afrika Mashariki imeshuhudia pia wabunge wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EALA), wakishindwa kufanya kikao cha Bunge hilo baada ya kutolewa hoja kuwa umefika wakati kwa wabunge wa Bunge hilo kufanya mikutano yao kwa kuzunguka nchi husika.

Hoja hiyo inaonekana ni mwendelezo wa kulipa kisasi dhidi ya Tanzania kwani ukiondoa wabunge wanaowakilisha nchi hii, wabunge kutoka Rwanda, Kenya, Uganda na Burundi wameamua kuunga mkono licha ya kwamba haikuwa sehemu ya ajenda ambayo itajadiliwa kwenye kikao hicho.

Akizungumza kwenye kikao hicho hivi karibuni, Mbunge kutoka nchini Kenya Peter Mathula, aliamua kuwasilisha hoja binafsi akitaka kutenguliwa kwa uamuzi wa vikao vya Bunge hilo kufanyika tu mjini Arusha Tanzania.

Vikao hivyo vimekuwa vikifanyika Arusha nchini Tanzania ambako ndiko makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mbunge huyo alijenga ushawishi kwa wabunge wa Bunge hilo, kukubali vikao hivyo kufanyika kwa mzunguko katika maeneo ya nchi hizo zinazounda Jumuia hiyo.

Hata hivyo kuwasilishwa kwa hoja hizo, kulizua malumbano huku wabunge wa Tanzania wakionekana pekee wakiipinga hoja hiyo.

Mbunge wa EALA kwa upande wa Tanzania Abdullah Mwinyi, aliongoza wabunge wa Tanzania kutoa nje ya ukumbi wa Bunge na kususia kikao hicho.

Hatua ya wabunge wa nchi zote zinazounda Bunge hilo kuwa na umoja wa kupinga vikao hivyo kufanyika Tanzania, imetafsiriwa kuwa ni mwendelezo wa mpango wa kuvuruga umoja uliokuwapo hapo awali.

Hata hivyo, baada ya mvutano huo, kikao cha uongozi wa Bunge hilo, kilifikia makubaliano ya vikao hivyo kufanyika kwa mzunguko.

Bunge la Tanzania kutokana na uhusiano tete kati ya Tanzania na Rwanda, wiki hii limeamua kuomba msimamo wa Serikali ya Tanzania ili kujua namna ambavyo limejipanga kutafuta suluhu.

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe aliitaka Serikali kuelezea msimamo wake hasa kutokana na kuonekana Rais Kagame hakufurahishwa na ushauri wa Rais Kikwete ambapo Waziri Mkuu Pinda wakati anatoa msimamo alisema Serikali ya Tanzania inaamini busara itatumika kupata ufumbuzi wake.

Pinda alisema Rais Kikwete ameeleza kwa kina kuhusu chanzo cha kutokuwepo kwa uhusiano mzuri na Rwanda , lakini bado alifafanua kuwa tayari Rais Kikwete amemuomba Rais Museveni kusaidia kupata kwa ufumbuzi wa suala hilo.

“Serikali tuaamini kuwa tutamaliza suala hilo kwa kutumia busara zaidi.Tunatambua heshima yetu kwa nchi za Afrika Mashariki na kubwa zaidi tumekuwa wasuluhishi wazuri wa migogoro kwenye nchi za Afrika Mashariki.Hivyo busara itatumika kupata suluhu,”alisema Pinda na kuongeza “Serikali hatutapuuza haya yanayoendelea,”.